Pages

Friday, 23 May 2014

TANZANIA COLLEGE FESTIVAL 2014: YALIYOJILI KATIKA TAMASHA HILI LILILOFANYIKA CHUO KIKUU MZUMBE MBEYA CAMPUS COLLEGE 17/05/2014

Asubuhi ya siku ya Tukio watu wakiwa katika harakati za maandalizi ya mwisho ya Tanzania College Festival


Moja ya waandaaji wa Tanzania College Festival 2014 Ndugu Brown akiwa katika majukumu ya kukamilisha maandalizi

Joan Kiggundu naye hakuwa nyuma

Diana Shumbusho moja ya Event organizer akikaguwa jambo kabla ya shughuli nzima haijaanza

Maonyesho ya wanafunzi toka Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya [MUST]
MUST walitia sana fora upande wa maonyesho

Maonyesho toka Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya

Mwakilishi toka NSSF akiteta jambo na wageni waalikwa kwenye maonyesho nje ya ukumbi wa tukio

Mwakilishi wa mgeni rasmi [RPC - MBEYA] Ndugu Samora akisikiliza kwa makini jambo toka kwa mwakilishi wa NSSF

Watu hawakuwa nyuma kuangalia maonyesho ya vyuo mbalimbali yaliyofanyika nje ya ukumbi wa NLT - Mzumbe

Moja ya waandaaji wa Tanzania College Festival Ndugu Baraka Dishoni akiteta jambo ndani ya ukumbi

Mwakilishi toka kampuni ya mtandao mpya wa mawasiliano SMART akitoa neno la utangulizi kabla shughuli haijaanza

Meza kuu ilipendeza vya kutosha





Wawakilishi toka Youth United Nations Association - YUNA nao walikuwepo kutoa support yao

Mwakilishi toka MUST katika kipengele cha QUIZ akijibu swali. MUST walichuana na MZUMBE UNIVERSITY na Mzumbe kuibuka kidedea

Mwakilishi toka Mzumbe katika kipengele cha QUIZ...Ndugu TESHA akijibu swali





Mhadhiri wa Chuo Kikukuu Mzumbe Ndugu John Stephen (Advocate) akiuliza swali kwa washiliki wa QUIZ Session



Baadhi ya waandaaji wa tamasha la Tanzania College Festival 2014 katika picha ya pamoja












Saturday, 3 August 2013

Kaburu: Nagombea Uenyekiti Simba

 
ALIYEKUWA Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ amesema kuwa anafikiria kugombea uenyekiti wa klabu hiyo katika uchaguzi ujao.
“Kweli mimi si kiongozi wa Simba kwa sasa, lakini ni mwanachama wa Simba na kikatiba nina haki ya kuendelea kuitumikia klabu yangu bila kipangamizi chochote hata kuwa Mwenyekiti wa klabu, haimanishi mimi kujiuzulu ndio mwisho wa kuwa kiongozi katika Simba, katiba hainizuii hivyo naweza kurudi na kuifanyia kitu klabu yangu kama kiongozi.”
Kaburu alisema kujiuzulu kwake kama kiongozi ilitokana na kutaka kupumzika na  kujipanga upya.
 “Watu wasiwe na hofu, ninakuja upya na wakati huu nitaangalia matatizo mbalimbali na kuyasuluhisha ili klabu kama klabu ifanikiwe,”alisema.
“Sasa nimetoka kwenye uongozi, nafikiri bado mimi mwanachama wa Simba naruhusiwa kutoa maoni yangu au hata saa zingine kuisaidia Simba kwenye mambo mbalimbali,” alisema Kaburu, ambaye kuonekana kwake mazoezi katika siku za karibuni kuliibua mjadala kwa mashabiki.

Huu ndio Upande wa Pili wa Suarez wa Arsenal

 


Hii ni kwa shabiki wa Arsenal. Hebu kaa kimya, kwa sekunde chache tu, kisha jiulize. Ingekuwa vipi Luis Suarez angekuwa Arsenal kwa sasa? Ungetaka abaki, au aende zake huko anakohitajika? Usijibu.
Mengi yanasemwa katika kipindi hiki, hasa baada ya Arsenal kupeleka ofa ya pauni 40,000,001 Liverpool, wakimtaka straika huyo, Suarez. Hakuna shaka, shabiki yeyote wa Arsenal ni mtu mwenye furaha kubwa kwa sasa kwasababu klabu yao inafukuzia usajili wa moja ya wanasoka wenye vipaji kwenye soka la kisasa.
Na zaidi ya hilo, Suarez amekuwa fundi mzuri wa kufunga mabao. Anafanya hivyo kila anapocheza. Lakini, linapokuja suala la kutaka kumsajili, Arsenal pamoja na furaha yao yote, inapaswa kujiuliza maswali ya msingi. Anafaa au usajili wake unataka kufanywa kwa kujikosha tu kwa watu kuwa nao wanasajili wachezaji wenye majina?
Ingekuwa vipi, Suarez kwa sasa angekuwa mchezaji wa Arsenal na analazimika kuhama? Tena angekuwa analazimisha kuhamia kwa timu kama Manchester City? Msimu uliopita, Robin van Persie alihamia Manchester. Mashabiki wengi sana wa Arsenal walikasirishwa na hilo, kwa sababu moja tu. Walimvumilia wakati wa majeruhi, walimsapoti kwa kila kitu na kisha akawaacha na kwenda kwa wapinzani, Manchester United. Haikuwa vizuri kwa mashabiki wa Arsenal kwa uamua wa kuhamia Manchester United.

Na mbaya zaidi alifanya hivyo baada ya msimu mmoja kucheza kwa kiwango kikubwa, bila ya kusumbuliwa na majeruhi yoyote. Hili halina tofauti sana na hadithi ya Suarez. Misimu miwili iliyopita, Suarez amekuwa mtuhumiwa wa matukio ya utovu wa nidhamu ndani na nje ya uwanja, lakini bado klabu yake ilimsapoti kwa kila hali. Baada ya kuandamwa na vyombo vya habari, straika huyo aliibuka na wazo la kutaka kuhamia ng’ambo ya nchi.
Lakini, baadaye akadai kwamba anataka kujiunga na timu itakayompa nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya bila kujali kama itakuwa ndani ya England au la. Kesi ya Suarez ipo tofauti na ya Van Persie, mshambuliaji huyo wa Uruguay ni mbinafsi, anajifikiria yeye zaidi. Kwa tabia yake hiyo, Arsenal wanapaswa kujiuliza kabla hawajatoa pesa yao nyingi kumsajili.
Arsene Wenger hapaswi kusahau kwamba ni Real Madrid, ambayo ni chaguo la kwanza la Suarez. Si Arsenal. Pia fikiria hili, Suarez ametua Arsenal, akaisaidia kutwaa taji la Ligi Kuu na kisha akafunga mabao 30. Unadhani kuna uhakika atabaki Arsenal mchezaji huyu? Mchezaji ambaye mapenzi yake ya kwanza yapo kwingine? Anadhani atazikataa Real Madrid na Barcelona zitakapokuja na ofa zao kutaka kumsajili?
Suarez ni mchezaji mahiri kweli, hilo halina pingamizi. Lakini, kwanini Wenger hakumsajili mchezaji huyo wakati alipokuwa Ajax. Kwa shabiki wa Liverpool uhamisho wake utamfanya kuwa na hasira, kwa sababu anahama baada ya kupata sapoti kubwa ya matatizo yake yenye utata. Kwa upande wa Arsenal, ukiweka ushabiki pembeni, kumsajili Suarez ni kujiweka katika hali ya hatari. Ikumbukwe, atahamia hapo akiwa na adhabu ya kukosa mechi sita. Je, kuna uhakika kwamba amepona ugonjwa wake na hatamng’ata mchezaji mwingine atakapokuwa ndani ya jezi za Arsenal?
Je, hatakumbana na adhabu ndefu wakati atakapotua Emirates? Je, hataamsha tena sakata la kutaka kuhama baada ya misimu miwili hasa ukizingatia mapenzi yake si kuichezea Arsenal? Kwa Suarez, Arsenal inajitengenezea bomu, itamsajili kwa pesa nyingi na kisha baada ya miaka miwili ataomba kwenda Barcelona au Real Madrid. Sawa, humtarajii Suarez azekee Emirates, lakini itakuwa hasara kama ataomba kuondoka baada ya misimu miwili.
Huu ndio wasiwasi  wa kuwa na mchezaji kama Suarez, ana uwezo lakini hakupi uhakika wa kuwa na mipango ya kujenga timu kupitia yeye. Real Madrid na Barcelona bado zitaendelea na chokochoko zao za kumsajili kama ataendeleza makali yake atakapotua Emirates.   
     
Kwa kiwango cha Suarez, kama hajapata tatizo la majeraha, suala la kung’ara hilo halina mjadala. Unatarajia kuliona kutoka kwake. Hakuna ubishi Arsenal itakuwa imepiga  bao watakapoinasa huduma yake, lakini tatizo lake ni moja tu. Haaminiki, hakawii kuchafua hali ya hewa. Hili ndilo lililopo upande wa pili wa sarafu katika usajili wa Suarez Arsenal.

source: mwanaspoti.co.tz



Friday, 12 July 2013

Brendan Rogers: Liverpool haitakiwi kumuuza Suarez anayewamiwa na Arsenal

Meneja wa klabu ya Liverpool amesisitiza kuwa timu hiyo haitakiwi kumuuza Luis Suarez anayewaniwa na Real Madrid pamoja na Arsenal.

Mchezaji huyo ambaye amekuwa akiongelea suara lake la kuhama kwenye timu hiyo karibu kipingi chote cha mapumziko ya ligi kuu yanayoendelea mpaka sasa amkekuwa akitakiwa na vilabu mbalimbali barani ulaya huku Real Madrid ikiwa ndiyo sehemu inayoonekana kumfaa zaidi mchezaji huyo mwenye miaka 26.

Hata hivyo kocha wa Arsenal mfaransa Arsene Wenger naye ameonekana kuvutiwa sana na mchezaji huyo kiasi cha kuwa na mpango wa kuongeza dau zaidi ya lile la paundi 30 elfu alilotuma mwanzao na kukataliwa na Liverpool.

Mchezaji huyo wa Uruguayi ameonekana na nia ya kutaka kuondoka klabuni hapo kwa kisingizio cha kuchoshwa na jinsi vyombo vya habari vya uingereza vinavyotaka kuuza kwa sababu ya kufuatilia maisha yake, lakini hivi karibuni mwakilishi wa mchezaji huyo alisema kuwa mchezaji huyo anataka kucheza kwenye timu inayoshiriki Champions Ligi msimu ujao.

"kwa miezi kadhaa sasa kumekuwa na hizi tetesi zikimhusisha Luis kuondoka Anfield lakini ukweli unabaki palepale kuwa Luis bado ni mchezaji wa Liverpool tunamjali na kutambua mchango wake kwenye timu iwapo uwanjan hata nje ya uwanja pia....nimeongea nae mara kwa mara kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno na kwa simu pia kuhusu tetesi hizi na ukweli unabaki palepale kuwa tunamheshimu sana Luis.." Brendan Rogers alikiambia kituo cha Radio cha TalkSPORT

Chelsea pia imeonekana kumwania mchezaji huyo ingawa kocha wa timu hiyo Jose Morinho ameonekana kuwekeza nguvu zake nyingi kwa mshambuliaji wa Kiingereza na timu ya Manchester United Wyne Rooney

Wednesday, 1 August 2012

MAELEZO BINAFSI YA MHE. ZITTO ZUBERI KABWE DHIDI YA TUHUMA ZA RUSHWA HUSUSAN KUELEKEA KATIKA KUPITISHA BAJETI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI

Ndugu Waandishi,

Nalazimika kukutana nanyi kutoa maelezo juu ya tuhuma zenye shinikizo la kisiasa zinazoelekezwa kwangu binafsi kwamba hata mimi nimeshiriki katika vitendo vya rushwa, kwa nafasi yangu kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma. Taarifa hizo, kama kawaida ya uzushi mwingine wowote  zimesambazwa kimkakati na kwa kasi kubwa kiasi cha kuukanganya umma.
Nafahamu nabeba dhamana kubwa ya uongozi, taswira yangu ya uongozi daima imeakisi njozi na matumaini ya wananchi wa Kigoma Kaskazini, wananchi wanyonge na vijana kote nchini bila kujali itikadi zao za kisiasa, jinsia zao, makabila yao na rika zao. Hivyo, nawajibika kupitia kwenu kuwatoa hofu juu ya hisia potofu zinazopandikizwa kwao na wale wasiopenda kuona baadhi yetu tukiwaunganisha na kuwasemea watanzania wasio na sauti, dhidi ya vitendo vya hujuma na vyenye dhamira ovu kwa taifa.
Mkakati huo wa kuniunganisha na baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wanaotuhumiwa kwa kupokea Rushwa unatekelezwa kwa njia zifuatazo:
  1.   Kumekuwa na kauli za watendaji wa serikali ambao wamekuwa wakizieneza na hususan kutoa taswira kwamba baadhi ya kauli zangu zinatokana na ushawishi wa rushwa;
  2.   Kuna taarifa ambazo zimeandikwa tena katika kurasa za mbele za baadhi ya vyombo vya habari  zikidai ’’Zitto kitanzini’’ ama ’’Zitto sawa na popo nundu’’  zikiashiria kwamba na mimi ni mla rushwa; na
  3.   Waandishi wa habari na jamii kwa ujumla wamefikia kuaminishwa habari hizi kiasi cha wengine kuuliza kwa nini Mhe. Zitto Kabwe hakutajwa katika orodha iliyotolewa na Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani.
Ndugu Waandishi,
Naomba kutoa ufafanuzi wa hicho kinachoelezwa kwamba nina ushiriki katika masuala ya rushwa hususan kwenye masuala yanayohusu sekta ya Nishati na Madini:-
  1. Mara baada ya bodi ya Wakurugenzi ya  Shirika la Usambazaji wa Umeme Tanzania (TANESCO) chini ya Uenyekiti wake Meja Jenerali Mstaafu Robert Mboma kutangaza kwamba imemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Nd. William Mhando ili kupisha uchunguzi wa baadhi ya vitendo/mwenendo wake, Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) ambayo mimi ni Mwenyekiti wake ilimuandikia Mhe. Spika kumuomba aridhie ili Kamati iweze kuwaita Bodi ya TANESCO, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali  (CAG) na pia Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kujiridhisha na tuhuma zote zinazotajwa zinafanyiwa uchunguzi wa kina na hatua kuchukuliwa;
  2. Kamati ya POAC ninayoiongoza ilimuomba Mhe. Spika kuwaita wahusika tajwa kwa kuwa zilikuwapo tetesi kuwa kusimamishwa kazi kwa Mkurugenzi huyo siku chache kabla ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kulikuwa na lengo la kufunika ’madudu’ makubwa zaidi kwa kulichagiza Bunge na tukio hilo dogo, mkakati ambao naona umefanikiwa sana. Isitoshe, Kamati kutaka kujiridhisha na hatua za Bodi ni sehemu ya msingi ya utekelezaji wa majukumu ya Kamati yaliyowekwa kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge na pia Shirika la TANESCO ni moja kati ya mashirika ambayo yanawajibika kwetu kwa hesabu zake na pia ufanisi wake kwa ujumla. Tumefanya hivyo pia katika mashirika mengine, hili la TANESCO sio tukio la kipekee;
  3. Kitendo hiki cha halali na kwa mujibu wa Kanuni kilichofanywa na Kamati yangu  kimetafsiriwa kwa makusudi na baadhi ya watu kwamba ni ishara ya kuwa sisi au zaidi kwamba mimi nina maslahi binafsi na TANESCO na hususan Mkurugenzi wake Injinia Mhando, ndio maana tumetaka maelezo ya Bodi. Ukweli kwamba Kamati ya POAC tumewaita pia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu (CAG) na Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kwa jambo hilo hilo umefichwa kwa makusudi!
  4. Baada ya  tukio hilo, nikiwa hapa Dodoma, mwandishi wa habari wa gazeti moja alinifuata akiniambia kuwa wamekutana na Mhe. Waziri Mhongo na Katibu Mkuu wake, Nd. Eliachim Maswi hapa hapa Bungeni na wamewaambia kuwa mimi nimepewa rushwa. Hakutaja nimepewa rushwa na nani, kiasi gani na wala kwa lengo gani!
  5. Nimejaribu kumtafuta kwa simu Mhe. Waziri Mhongo na Katibu Mkuu wake ili wanipe ufafanuzi juu ya mimi na Kamati ya POAC kuhusishwa na tuhuma hizi bila mafanikio, hali ambayo inaniondolea mashaka juu ya ushiriki wao katika kueneza au kuthibitisha uvumi huo. Najaribu sana kujizuia kutokuwa na mashaka na ushiriki wao huo ikizingatiwa uzito na taswira ya nafasi zao katika jamii, lakini wameshindwa kunidhihirishia tofauti.
Sasa naomba kutoa ufafanuzi rasmi kuhusu mlolongo wa matukio hayo tajwa ambayo yanatumiwa na baadhi ya wanasiasa kuonesha kwamba eti nimehusika na vitendo vya rushwa.
  1. Binafsi sijawahi kuwa na mawasiliano ya aina yeyote na uongozi wa TANESCO kushawishiwa juu ya hatua ambazo POAC ndio imezichukua za kutaka kujiridhisha juu ya utaratibu uliotumika. Ieleweke wazi kabisa kuwa, hakuna wakati wowote, popote ambapo mimi binafsi au Kamati yetu imekataa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO kuchunguzwa kwa tuhuma zozote. Ambacho tumesisitiza wakati wote ni ufuatwaji wa taratibu, kanuni na sheria, hili nitalisimamia iwe masika au kiangazi;
  1. Ni kwa sababu hiyo, na kwa kujiamini kabisa nimeunga mkono suala la tuhuma za rushwa zinazotajwa zichunguzwe na Kamati ya Haki, Maadili na  Madaraka  ya  Bunge kwa kina;
  1. Nimekwenda mbali zaidi kukiomba chama changu CHADEMA kifanye pia uchunguzi na tathmini yake kwa kina kujiridhisha na tuhuma hizo;
  1. Natumia fursa hii pia kuomba vyombo vya Dola vichunguze tuhuma hizo kwa nafasi yake ili kuweza kupata ukweli;
  1. Ninaahidi kushiriki kikamilifu iwapo nitatakiwa katika uchunguzi wowote utakaofanywa na niko tayari kuwajibika iwapo nitakutwa na hatia yeyote.
Napenda niwatoe hofu wananchi wa jimbo la Kigoma Kaskazini walionituma kuja kuwawakilisha hapa Bungeni na Watanzania wote kwa ujumla kwamba:-
  1. Mimi Zitto Zuberi Kabwe sina bei, sijawahi kuwa nayo na sitarajii kuwa nayo huko mbeleni. Daima nimesimamia kidete maadili ya uongozi bora katika maisha yangu yote ya siasa, na nawaahidi sitarudi nyuma katika mapambano dhidi ya rushwa katika nchi hii pamoja na mikakati ya aina hii ya kunidhoofisha na kunivunja moyo;
  1. Nafarijika na salam mbali mbali zinazotolewa kunifariji na kusisitiza kuwa nisilegeze kamba katika mapambano haya, nimepokea ujumbe mwingi kwa simu, sms, tweeter na hata facebook na niko pamoja nanyi Watanzania wenzangu kamwe sitarudi nyuma hadi kieleweke. Naamini katika nchi yetu tunazo rasilimali za kutosha mahitaji/haja ya kila mmoja wetu lakini si ‘tamaa/ulafi’ wa baadhi ya watanzania wenzetu;
  1. Napenda kuweka rekodi sawa kwa Watanzania kwamba nimekuwa Mbunge hiki ni kipindi cha pili, Mimi ni Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) huu ni takriban mwaka wa saba sasa, Kamati yangu inasimamia mashirika 259 ya Umma na si TANESCO peke yake. Mchango wa Kamati hii katika Bunge na kwa ustawi wa Mashirika ya Umma ni bayana na haujawahi kutiliwa shaka. Kamati yetu imeokoa upotevu mkubwa wa mali za umma na kuokoa fedha za umma kutokana na umakini wake. Tumefanya hivyo CHC hivi karibuni, Kiwira na kwenye mashirika mengine mengi. Kote huko uadilifu na uzalendo wa Kamati hii haujawahi kuhojiwa. Inatuwia vigumu kuona kuwa tunahojiwa katika suala hili la TANESCO. Hapa pana kitendawili.
  1. Zipo hoja pandikizi za kutaka Kamati ya POAC ivunjwe na haswa zikinilenga mimi binafsi. Nafahamu kiu ya wasioitakia mema nchi yetu kuiona POAC ikivunjwa au sura zikibadilishwa kwa kuwa Kamati hii imekuwa mwiba kwa mikakati yao ya kifisadi. Kwa maoni yangu, Kamati ya POAC isihusishwe na tuhuma hizi kwa vyovyote vile. Niko tayari nihukumiwe mimi kama mimi na sio kuhusisha wajumbe wengine ambao hawatajwi mahala popote katika tuhuma hizi mbaya sana katika historia ya Bunge letu. Nitakuwa tayari kunusuru Kamati ya POAC na maslahi ya taifa letu kwa kujiuzulu Uenyekiti iwapo itathibitika pasipo shaka kuwa nimehongwa. Kamati ya POAC ni muhimu zaidi kuliko mimi.
  1. Nafahamu pia kuwa kuna wanasiasa hasa wa Upinzani ambao wanautaka sana Uenyekiti wa POAC na wanafanya kila njia kutaka kuidhoofisha. Lakini hawajui kuwa anaepanga wajumbe wa Kamati ni Spika wa Bunge.
  1. Msishangae pia kuja baadae kubaini kwamba baadhi ya wanasiasa wenye midomo mikubwa ya kutuhumu wenzao wao ndio vinara wa kupokea rushwa.
  1. Ni lazima tufike mahali kama viongozi kwamba utaratibu unapokiukwa na yeyote yule, au uongo unapotolewa hadharani tuseme bila kuogopa. Hili ndio jukumu letu kama wabunge na viongozi. Kusimamia ufuatiliaji wa utaratibu ni jukumu letu kama Kamati ya POAC na ndio sababu ya msingi ya kuanzishwa kwa mamlaka kama CAG na PPRA. Haiwezekani, tuwe na set ya kanuni kwa kundi fulani na nyingine kwa makundi mengine, au kuhukumu ufuataji wa taratibu kwa kuangalia sura ya mtu usoni
Mwisho
Kumejengeka tabia hivi sasa ya kuwamaliza wanasiasa wenye kudai uwajibikaji na uzalendo. Kumeanzishwa kiwanda kwenye medani ya siasa cha kuzalisha majungu na fitna zenye lengo la kuwachonganisha wanasiasa wa aina hiyo na wananchi kwa kutumia vyombo vya habari na nguvu ya fedha. Naamini mbinu hizi chafu, kama nyingine nyingi zilizojaribiwa kwangu huko nyuma nazo zitashindwa.

Naamini katika kweli na kweli daima huniweka huru. Naamini kuwa mwale mdogo wa mwanga wa mshumaa hufukuza kiza. Kwa imani hiyo, sitasalimu amri mbele ya dhamira zao ovu hata nitakapobaki peke yangu katika mapambano hayo ya kulinda na kutetea rasilimali za taifa zinufaishe watanzania wote.

Daima nitaongozwa na busara ya Hayati Shabaan Robert isemayo, ‘Msema kweli huchukiwa na marafiki zake, nitakapofikwa na ajali hiyo, sitaona wivu juu ya wale wawezao kudumu na marafiki zao siku zote, siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo, nikajitenga na furaha ya kweli itakayotokea pale uwongo utakapojitenga”.

Ahsanteni sana.

JUA SAKATA LA NGASSA NA UHAMISHO WAKE TOKA AZM

Kidogo niongelee soka la bongo japo kuwa sio mzoefu sana lakini haya ndio mawazo yangu.
 
Timu kubwa nchini ni Simba Sports Club na Dar Es Salaam Young African tukubali, ni kweli Azam FC imekuja na kuleta changamoto si kwa timu hizi bali kwa ligi kama msimu uliopita, lakini kwangu mimi nimeona kuwa kidogo ndugu zetu Azam walijisahau kuwa Simba na Yanga bado ni timu kubwa na wao ndio kwanza wanaanza kupanda. Sawa nakubali kabisa kuwa Azam iko well Organized, lakini the way kwa tathmini fupi niiyoiona katika mashindano ya kombe la Kagame hasa baada ya wana rambaramba kuiondoa Simba Sports club kwa mabao 3 kwa 1, walijiona wamemaliza kila kitu hali iliyopelekea kuleta dharau na kejeli na baadhi ya wadau kuanza ku-support kejeli zile, ilifikia wakati timu hizi Simba na Yanga zikifananishwa na mapacha wawili yaani "Kulwa - Yanga, Doto - Simba" na aliyebuni majina haya ni mtu wa soka na mpenda soka na kufanya kuzidi kupelekea jeuri na kujiamini kabisa "Kulwa na Doto" zitakuwa chali.

 Tatizo kubwa nililoliona hapa ni kwa wana rambaramba walidhani timu hazibadiliki kimchezo kama Azam {waanayoona iko well organized} Azam wana malengo mazuri sana kuhusu timu yao lakini uwezo wa kiufundi ndo umeishia pale. Nilikwambia siku ile waliyocheza na Vita kwamba Azam hawana plan B, na ndicho kilichojitokeza mechi ya fainali. Wanacheza formation moja, hawawezi kubadilika kutokana na mchezo
 
Ninavyohisi "sina uhakika kwa hili lakini kutokana na maneno ya wapenda soka, na lisemwalo lipo kama halipo?"  Hata wenyewe wanasema wako modern but wanapita mulemule zinapopita Simba na Yanga.
 
Kuna mtu aliniambia "Tangu lini club ikatoa tuzo kwa waandishi wa habari? Kama sio wanatengeneza mazingira ya kuwasifia hata kama wanafanya madudu! Azam nakubali wana malengo mazuri lakini njia wanazopita nao ni utata!" nilimbishia lakini ujumbe wake ulinifikia

Suala la Mrisho Ngasa kuvaa jezi ya Yanga,  kwangu mie naona wote wana makosa, Ngassa ameshindwa kutambua mpira ndio kazi yake na Azam ni mwajiri wake,  na Azam nao pia wameshindwa kuibadili mind ya Ngasa ili ajisikie yuko nyumbani. Kama mlimchukua kwa ajili ya kuleta mafanikio kwa klabu na mnaona anawaza kule alikotoka lazima mkae nae na mumuondoa kule ajisikie huku alipo sasa kuna ubora pia, ninaamini ipo siku Ngassa atafunguka kwanini alikubali kuvaa jezi ya Yanga inawezekana ni kweli kutokana na mapenzi aliyonayo kwa klabu ya Yanga lakini ile siku ya hili tukio wadau walimtaja mchezaji mwingine wa wana rambaramba kuwa yeye amekulia Yanga kabisa lakini walimpongeza wa kutokufanya kama Ngassa yaani kujionyesha hadharani, lakini pia tunaweza mlaumu Ngassa kwakua hatujui upande wa pili wa shilingi, sakata hili wanaoweza kutuondoa katika matongotongo ni Ngassa na Azam FC.

Kuna wachezaji wala mie naona hawastahili kupata namba lakini utashangaa wanapata #. Hivi Hamis Mcha ni mtu wa kumweka Ngassa benchi?   Kiwango cha George Odhiambo "Blackberry" kinaendana na sifa alizokuwa anapewa? au siku zile Blackberry ilikuwa Whiteberry?

Kiongozi wa klabu anaandika post Facebook za kuponda na kukashifu timu nyingine na kuona anayofanyia kazi ni bora sana hali inayofanya anakiuka hata taratibu za kazi na wadhifa alionao.

Wasipoangalia wataishia kuwa na viwanja vizuri, gym, hostel nzuri lakini kiuwezo wa uwanjani wakabaki vilevile.

Kiongozi anaongea na chombo cha habari anasema eti wachezaji Azam hawajazoea kucheza mbele ya watu weng ndio maana wamefungwa! Hivi Ngassa, Nyoni, Tchetche,Bocco, Sure boy, Shikanda , Blackbery na Agrey Moris hawajawahI kucheza mbele ya watu wengi? Ah hapa kachemka, aseme lingine.

Wanataka dola 50000, sawa inawezekana wanahitaji kurudisha gharama zao lakini isije ikawa ni kumkomoa Ngassa, na kuna tetesi kuwa wanataka kumpeleka Simba na kuifanyia Yanga fitna isimpate, ama ndio ile ishu tuendelee kuamini kuwa Simba Sports Club na Azam FC ni ndugu?

Ndio nasema unaweza kuwa na viwanja , apartments na gym nzuri lakini bado ukawa na team mbovu. Ukishindwa kwenye technical bench na kuijenga timu psychological ujue hauwezi kufika popote. Azam wanasema wako well organized lakini technically hawana tofauti na Simba na Yanga. Tofaut yao ipo kwny physical infrastructures tu.

Mwisho nawashauri Azam kwamba wajitahidi kuboresha na bench la ufundi pia, miundo mbinu yao haitasaidia chochote kama technical bench liko weak. Shule inaweza kuwa na kila ki2 {vitabu, madarasa, library nzuri} lakini isipokuwa na walimu bora wanaojua kumpa mwanafunzi maarifa na mbinu za kufaulu hiyo shule haiwezi kufaulisha.

Pia wawajenge wachezaji wao kisaikolojia ili wajione ni sehemu ya mafanikio ya Azam. Na ndio nasema hata Azam nao wana makosa, wameshindwa kumfanya Ngassa ajisikie yupo nyumbani, na kama wakiendelea kubaki na timu ile hawatafika kokote kwa sababu tangu Azam ya akina  marehemu Mafisango hadi hii ya leo haijabadlika chochote. Inacheza mpira uleule .

Huu ni mtazamo wangu mie, kila mmoja ana uhuru wa kutoa mtazamo wake na tupende kupata challenges.
 
source:shaffihdauda.com

Thursday, 28 June 2012

SERIKALI ITOE TAMKO JUU YA KILICHOMSIBU DK. ULIMBOKA

Dk. Ulimboka akiwa na majeraha baada ya kushambuliwa
Mbunge wa Nzega, Dk Khamis Kigwangala ameitaka Serikali kutoa majibu fasaha kuhusu kilichomtokea Dk Stephen Ulimboka akieleza kuwa kilichomtokea kiongozi huyo wa madaktari kinasikitisha. Dk Kigwangala alisema hayo jana alipozungumza na gazeti hili kuhusu tukio lililomkuba Dk Ulimboka.

Alisema kuwa ni muhimu kwa Serikali kufanya hivyo kwa kuwa Dk Ulimboka alikuwa katika harakati za kudai haki za madaktari ambapo kabla hawajafikia azma yao  amekutwa na jambo la kusikitisha.

 “Ukimwangalia picha zake huwezi kumtambua, tumefikia mahali kitu kama hiki kinatokea, inasikitisha sana. Kuna haja kwa Serikali kuthibitisha kuwa haijahusika kwa tukio hilo kwani taarifa silizosambaa zinaeleza kuwa imehusika,”alisema Dk Kigwangala. Alisema ni lazima Serikali iwajibike kwenye suala hilo ingawa haamini kama inaweza kufanya tukio kama hilo.

Dk Kigwangala alisema taarifa zilizopo ni kwamba Daktari huyo alipigiwa simu na mtu wa Serikali ili kuangalia namna gani wanaweza kuzungumzia kusitisha mgomo huo. Akizungumzia historia ya Dk Ulimboka alisema kuwa  ni mtu mwenye msimamo mkali na asiyependa kuyumbishwa waliyekutana Chuo Kikuu cha Tiba Muhimbili (MUHAS) mwaka 1998 walipokwenda kusomea udaktari.
Alisema kabla ya Dk Ulimboka kujiunga na MUHAS alitokea Shule ya Sekondari Mzumbe ambapo alikuwa amesomea mchepuo wa Sayansi(PCB).

UHISPANIA YATINGA FAINALI ZA EURO 2012 NCHINI POLAND & UKRAINE

game ilipigwa kwa dakika 120
Mabingwa watetezi Uhispania wamefuzu kuingia fainali ya Euro 2012, baada ya kuishinda Ureno magoli 4-2, kupitia mikwaju ya penalti, baada ya muda wa kawaida wa dakika 90 na dakika 30 za ziaida kumalizika kwa timu hizo mbili kushindwa kufungana.
Bao la mwisho la mikwaju ya penalti kwa Uhispania lilitiwa wavuni na Cesc Fabregas, na kuwapa wenzake matumaini ya kutetea ubingwa wao kikamilifu, watakapocheza aidha na Ujerumani au Italia katika fainali ya Jumapili.
Fabregas, ambaye ni kiungo cha kati wa timu ya Barcelona, alipiga mkwaju ambao baada ya kugonga mwamba upande wa kushoto, ulitambaa wavuni, na ikawa ni tiketi ya Uhispania kufanya mipango ya kusafiri hadi Kiev, Ukraine, kwa fainali.
Mchezaji wa Ureno, Bruno Alves, alielekea kuwa na wasiwasi, na kushindwa kufunga mkwaju wake, baada ya mpira kugonga mwamba, na Ronaldo, akiwa amepangwa na timu yake katika nafasi ya tano kwa wapigaji penalti, hakupata hata nafasi ya kutimiza wajibu huo.
Wengine waliokosa kufunga kupitia mikwaju ya penalti ni mchezaji wa Ureno, Joao Moutinho, wakati kipa wa Uhispania, Casillas, alipoweza kuokoa kwa kuruka upande wa kkulia.
Awali mchezaji wa Uhsipania Xabi Alonso naye alikosa kutumbukiza wavuni mkwaju wa penalti, licha ya kwamba ulikuwa ni mkwaju wa kasi na uliopigwa kwa nguvu, lakini kipa Rui Patricio akauzuia.

Wednesday, 13 June 2012

DI MATTEO ASAINI MKATABA WA MIAKA MIWILI KUINOA CHELSEA

Kocha aliyechukua mikoba kwa muda baada ya kufukuzwa kwa Andres Villa Boas Chelsea, Di Matteo amesaini mkataba wa miaka miwili kukinoa kikosi hicho tokea jijini London.

Di Matteo, 42 alichukua jukumu la kuinoa Chelsea kwa mkataba wa muda mfupi baada ya aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo kufukuzwa kazi. Di Matteo alishinda vikombe viwili akiwa kama kocha wa muda wa Chelsea, Kombe la FA Cup na lile la Klabu Bingwa barani Ulaya.

Mchezaji huyo wa Italy pia Chelsea mapema jumatano hii baada ya kutangazwa kuwa kocha wa kudumu amesema "Nina furaha sana kuchaguliwa kama kocha mkuu wa kikosi cha kwanza"

"Wote kwa pamoja tulipata mafanikio makubwa msimu uliopita kitu kilichoweka historia kwa klabu hii kubwa duniani. Lengo letu ni kuendeleza kile tulichokipata na nimejiandaa vizuri kwa ajiri ya maandalizi ya msimu ujao" aliongeza kusema Di Matteo

Uwezo wa Di Matteo umeweza kuonekana baada ya kuifanya Chelsea kuwa klabu ya kwanza toka jiji la London kuweza kushinda kombe la UEFA Champions League.

MATUMAINI YA MASHABIKI WA UHOLANZI KABLA YA MECHI NA GERMANY


Mechi imemalizika kwa Uholanzi kupokea kipigo cha 2-1 toka kwa Wajerumani a.k.a roho ya paka, magoli ya Germany yakifungwa na Super Mario Gomezi huku lile la kufutia machozi toka kwa Uholanzi likifungwa na Van Persie

Tuesday, 12 June 2012

TFF YATOA RUKSA YONDANI KUCHEZA YANGA MSIMU UJAO

Yanga wakimtambulisha Yondani baada ya kusaini mkataba

Utata wa usajili wa Kelvin Yondani unaelekea kupata majibu mapema baada ya kuthibitika kuwa ataichezea Yanga msimu ujao. 

Mmoja wa wajumbe wa kamati mmojawapo ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) aliithibitishia Mwanaspoti jana Jumatatu kuwa Yondani atacheza Yanga msimu ujao baada ya kugundua udanganyifu uliofanyika Simba. 

"Hapa tuwe wa kweli. Simba wanasema walimsainisha Yondani Desemba mwaka jana, tunajua kuwa Yondani alikuwa na matatizo na Simba wakati huo angesaini vipi mkataba mpya?" Alihoji mjumbe huyo wa TFF. 

Mjumbe huyo alisema Simba wanaonekana kushindwa mapema katika kesi hiyo kwa sababu kama wangekuwa wanamtaka Yondani wangemsainisha kabla hajaingia miezi sita ya mwisho na mkataba wake ungesajiliwa TFF. 

"Hivi unadhani Simba wangekuwa wanamtaka Yondani wangesubiri mpaka mkataba wake uishe?" Alihoji. 

"Huyu sisi tuna taarifa kuwa alisaini Simba baada ya timu kurejea kutoka Algeria katika Kombe la Shirikisho. Ila walichokifanya ni kurudisha nyuma tarehe ya usajili ili ionekane amesajili Desemba. 

"Hata kama amesajili Desemba bado walichelewa kwa sababu wakati huo tayari Yondani alikuwa amebakiza mkataba wa miezi sita, hivyo alikuwa huru kusaini klabu yoyote. " 

Mwanaspoti ilipomuuliza Yondani atacheza timu gani msimu ujao alisema: "Kwa mazingira yote hayo ni dhahiri atacheza Yanga kwa asilimia mia." 

Familia ya Yondani 
Kaka mkubwa wa Kelvin Yondani ambaye pia ni wakala wa mchezaji huyo, Sunday Patrick ameridhia beki huyo kwenda Jangwani. 

Sunday aliiambia Mwanaspoti wiki iliyopita kuwa: "Sisi kama familia kwa moyo mmoja tupo na Yondani katika uamuzi wake, cha msingi yeye amefuata sheria na hana mkataba wowote na Simba ndio maana hata sisi tumempa baraka za kwenda Yanga, pia viongozi wa Simba wanapaswa kufahamu kuwa mchezaji huyu bado ni mdogo na anatafuta maisha hivyo wamuache afanye uamuzi wake." 

Kauli ya Yondani 
Yondani ambaye awali alidai kusaini Simba, Alhamisi iliyopita aliikana kauli hiyo na kusema amesaini Yanga. 
"Nimesaini Yanga, nawatakia kila la kheri Simba." 

Yondani amelamba Sh.30 milioni kutoka Yanga na atakuwa akilipwa mshahara wa Sh 800,000 ingawa kuna taarifa kuwa ameongezewa na atakuwa akilipwa Sh milioni moja kwa mwezi huku ikidaiwa Simba ilipanga kumpa Sh 25 milioni na angelipwa mshahara wa Sh 800,000. 

Kanuni ya TFF 
Kanuni ya 43 ya TFF ya masharti ya mikataba kati ya wachezaji na klabu kifungu cha 3 kinasema; " Klabu inayotarajia kuingia mkataba na mchezaji wa kulipwa haina budi kuiarifu klabu yake ya sasa kwa maandishi kabla ya kufanya makubaliano na mchezaji huyo wa kulipwa. 

Mchezaji wa kulipwa atakuwa huru tu kuingia mkataba na klabu nyingine iwapo mkataba wake na klabu yake ya sasa umekwisha au utakwisha baada ya miezi sita. Uvunjaji wowote wa sharti hili utastahili vikwazo vinavyofaa."

Tafsiri ya kanuni 
Kutokana na kanuni hiyo, Yondani alikuwa huru kufanya mazungumzo au hata kusaini mkataba na klabu yoyote tangu Desemba mwaka jana kwa sababu mkataba wake ulikuwa umebakiza miezi sita kwani umekwisha Mei 31 

Monday, 11 June 2012

MCHEZAJI WA ZAMANI WA ENGLAND NA KLABU YA EVERTON GORDON WEST AFARIKI AKIWA NA MIAKA 69

West mwenye jezi ya kijana akionyesha cheche zake
Mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya England na klabu ya Everton, Gordon West afariki dunia akiwa na miaka 69 baada ya kusumbuliwa na maladhi kwa muda mrefu.

West alikaa Goodison Park kwa miaka 11 huku akicheza michezo zaidi ya 400 na alifanikiwa kushinda mataji 2 ya ligi mwaka 1963 na 1970, pia kombe la FA mwaka 1966.

Everton ilimsajili Gordon West kwa kitita cha pound za Uingereza 27,000 kutoka Blackpool na kuweka rekodi ya goli kipa kusajiliwa kwa pesa nyingi kwenye ligi ya England.

Pia kipa huyo alipata kushinda vikombe vitatu akiwa na England, na alikuwa moja kati ya wachezaji wa kikosi cha England kilichoshika nafasi ya tatu kwenye michuano ya Ulaya mwaka 1968. Hata hivyo baada ya miaka miwili West alikataa kwenda Mexico kushiriki kombe la Dunia na timu ya taifa ya England kwa kisingizio cha kutaka muda wa kutosha kukaa na familia yake.

Gordon West pia alipata kucheza timu jirani na Everton, Tranmere Rovers

NIGERIAN POLICE RESCUE ABDUCTED FOOTBALLER OBODO


Mchezaji aliyekuwa ametekwa nyara Christian Obodo
Nigerian police have rescued Christian Obodo without the payment of a ransom demanded by his abductors.


Officers tracked his alleged abductors to Isoko, just outside Warri, on Sunday, where they found Obodo and arrested some suspects.
The midfielder was abducted by unknown gunmen near the oil city of Warri in southern Nigeria on Saturday.
The kidnappers had issued a ransom demand for nearly US$200,000 (£129,000).
Obodo, who was on loan at Italian side Lecce from rivals Udinese last season, was driving alone early on Saturday morning when he was abducted.
It is not the first time a footballer has been kidnapped in Nigeria.
International defender Onyekachi Apam was kidnapped by armed men who took his car before releasing him.
Nornu Yobo, elder brother of Everton defender Joseph, was famously kidnapped in 2008 in oil-rich Port Harcourt.
Nornu was released after 10 days but it was never made clear whether a ransom was paid.
Last year, the father of Chelsea midfielder John Mikel Obi was also seized in Jos, north-central Nigeria.
Nigerian police, however, rescued Micheal Obi senior from his abductors days later.

source: www.bbc.co.uk/football

MJUE MCHEZAJI WA KWANZA MWENYE ASILI YA AFRIKA KUCHEZA SOKA LA KULIPWA

Arthur Wharton
Shirikisho la Soka la Kimataifa, Fifa, limemtunuku Tuzo ya Mwanasoka wa Kwanza mwenye asili ya Afrika kucheza soka ya kulipwa, Arthur Wharton.


Fifa ilitoa tuzo hiyo kwa mchezaji huyo aliyekuwa akiichezea Darlington ya England. Shughuli hiyo ya tuzo ilifanyika Makao Makuu ya Fifa mjini Zurich.

Rais wa Fifa, Sepp Blatter, alisema kuwa shirikisho lake limefanya hivyo kuonyesha kuwa hakuna ubaguzi wa rangi katika soka.

"Hii ni siku muhimu kwa Fifa," alisema.

"Tunafanya kazi kupinga ubaguzi. Soka inaunganisha watu, inaleta watu karibu, na tunamtunuku kupitia Arthur Wharton Foundation," alisema Blatter. 

"Alikuwa mwanasoka wa kwanza mwenye asili ya Afrika kucheza Ligi Kuu England lakini tunajiuliza, imechukua muda gani hadi mchezaji mweusi kuitwa kwenye timu ya taifa ya England, ni kama miaka 100."

"Mwanasoka huyu tayari anafahamika Wembley na FA imechanga pauni 20,000 kama heshima yake Darlington katika mfuko wake wa maendeleo ya soka.

Wharton alikuwa raia wa Gold Coast (sasa Ghana), alikwenda England mwaka 1884, akiwa na miaka 19. Alikuwa na mpango wa kucheza soka katika klabu ya Methodist iliyoko Cleveland College, Darlington.

Mwaka 1886 alikuja kuwa mkimbiaji wa mita 100 na alishinda mbio hizo. Mwaka mmoja baadaye alishinda mbio za baiskeli zilizokuwa zikishindanwa kutoka Preston hadi Blackburn.

Uwezo wake katika michezo ulionwa na Klabu ya Darlington ambayo ilimsajili kama golikipa na aliidakia kuanzia 1885 hadi 1888 na kuwa Mwafrika wa kwanza kucheza soka ya kulipwa England. Alizichezea pia Preston North End, Stockport County na Sheffield United.

Mfanyabiashara na mmiliki wa Darlington FC, Shaun Campbell alimsajili Wharton kwa zaidi ya miaka mitano.

"Ni wazi kutambuliwa kwake na Fifa ni sehemu ya mafanikio na kunaupa nguvu mfuko wa Arthur Wharton," anasema Blatter.

Sunday, 10 June 2012

RESULTS: TANZANIA 2 - 1 GAMBIA


Vijana wa Kim Poulsen timu ya soka ya Tanzania maarufu kama Taifa Stars imepigana kufa na kupona leo kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya timu ya Taifa ya Gambia.

Gambia ndio waliokuwa wa kwanza kufunga goli lililowekwa kimiani mnamo dak. 7 ya mchezo na Ceesay, Taifa Stars walijitajidi kadri ya uwezo wao kusawazisha bao hili lakini kosakosa nyingi langoni mwa Gambia hazikuzaa matunda hadi kipindi cha kwanza kinamalizika.

Dakika ya 60 kipindi cha pili, Shomari Kapombe aliisawazishia Taifa stars kufuatia klosi nzuri iliyopigwa na Erasto nyoni ikitokea winga ya kulia.

Watanzania wakiwa na matumaini ya kupata ushindi walizidi kulisakama lango la Gambia mara baada ya kusawazisha goli lakini Wagambia hao walikuwa na safu nzuri ya ulinzi iliyowapa tabu sana vijana wa Tanzania.

Mnamo dakika ya 84 beki wa Gambia alinawa mpira kwenye eneo la hatari kufuatia klosi hatari iliyopigwa na Mbwana Samatta. Erasto Nyoni alipiga kwa ustadi mkubwa penati hiyo na kuiandikia Stars bao la 2 na la ushindi.

Mpaka sasa Stars inashika nafasi ya pili iliwa na pointi 3, pointi moja nyuma ya vinara Ivory Coast wenye pointi 4 baada ya kutoka sare hiyo jana na Morroco. Gambia wao wanashika mkia wakiwa na pointi 1 baada ya kutoa sare mchezo wao wa kwanza dhidi ya Morroco.

BREAKING NEWS: WAZIRI WA USALAMA NCHINI KENYA AFARIKI KWA AJALI YA HELKOPTA


Waziri Saitoti
Waziri wa Usalama wa ndani Profesa George Saitoti na Naibu wake Orwa Ojode wamefariki dunia katika ajali ya helikopta ya polisi iliyotokea leo asubuhi katika eneo la Kibiku, karibu na mji wa Ngong takriban kilometa ishirini kutoka mji mkuu wa Nairobi.
Abiria wote sita, wakiwemo marubani wawili na walinzi wa mawaziri hao waliokuwa kwenye helikopta hiyo wamefariki dunia na miili yao kuteketezwa kwa kiasi cha kutoweza kutambulika.
Kilichosababisha ajali hiyo bado hakijabainika.
Bwana Saitoti na maafisa wengine wa juu katika wizara ya usalama wa ndani walikuwa wakielekea katika eneo la Sotik kwa mkutano wa usalama. Saitoti alikuwa miongoni mwa wanasiasa mashuhuri nchini Kenya waliokuwa wakipania kugombea kiti cha urais katika uchaguzi mkuu ujao.
Walioshuhudia ajali hiyo wamesema waliona helikota hiyo ikizunguka angani kabla ya kuanguka katika msitu wa Ngong.
Polisi wamezingira eneo la ajali hiyo na kamishna wa polisi Mathew Iteere aliyepo katika eneo la ajali anatarajiwa kutoa taarifa kamili kuhusiana na ajali hiyo.
Ajali hiyo ya helikopta imetokea katika siku ambapo Kenya inaadhimisha miaka minne tangu kutokea ajali ya ndege iliyowauwa mawaziri wengine wa serikali, Kipkalya Kones na Lorna Laboso.

ARSENE WENGER AITAHADHALISHA ENGLAND KUELEKEA MCHEZO DHIDI YA UFARANSA


Arsene Wenger

KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger anaamini kufungwa kwa Ufaransa au England kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi D utaozikutanisha timu hizo utapoteza matumani yao Euro 2012.

England itavaa Ufaransa mjini Donetsk hapo Jumatatu mechi ambayo Wenger anaamini itaamua hatma ya kundi hilo lililokuwa na nyingine Sweden na wenyeji wenza Ukraine.

Wenger alisema hayo wakati wa mahojiano na tovuti ya Arsenal (www.arsenal.com) kuwa England wana kibarua kigumu zaidi baada ya kuwakosa nyota wake kadhaa wakiwemo Wayne Rooney ambaye amefungiwa kucheza mechi mbili za kwanza za nchi hiyo.
"Mechi ya ufunguzi kati ya England na Ufaransa na kukosekana kwa Rooney, unaweza kusema ni mchezo ambao hatakiwi kupoteza," alisema Wenger.

"Kwanini? Kwa sababu hutaweza kurudi kwenye mstari wa ushindani kutokana na presha kubwa kutoka kwa mashabiki wa nchi zao wanaotaka kuona timu yao ikishinda tu.
"Mechi hiyo itaamua hatma ya kundi lote. Kama ikimalizika kwa sare 0-0, hapo kundi litakuwa wazi kwa wote, lakini kama moja atafungwa atakuwa wamejifungulia njia ya kutolewa kwa sababu Ukraine itaifunga moja ya nchi hizo mbili na Sweden ni timu ngumu kufungika."

Wenger anaamini mchezo wa kwanza wa England ndiyo utakaoamua hatma yao wakiwa na kocha wao mpya Roy Hodgson.

"England watamkosa Rooney, wana kocha mpya na hawajakaa pamoja... ni vigumu kuwategeneza na kuwa timu kwa haraka," alisema.

"Unaweza kufanikiwa au hapana? Hiyo itajulikana baada ya mechi ya kwanza.
"Faida pekee kwa England ni kuwa na kocha mzoefu Hodgson aliyewahi kufundisha timu ya taifa na mwenye uzoefu na mashindano haya na mwenye kuwafahamu vizuri wachezaji wa England.


"Kwa sasa England bado wanaangaika kujenga kujiamini na kama wakifanikiwa kufanya hilo, basi wataweza kupata matokeo mazuri."

Wakati huohuo; Wenger anaamini Ufaransa ina uwezo wa kurudia mafanikio yake ya Euro 2000, lakini kama wachezaji wake wakiweka kado mawazo mabaya yaliyowakutaka kwenye fainali za Kombe la Dunia 2010.

"Wachezaji wa Ufaransa wanaweza kutwaa ubingwa wa fainali hizi," alisema Wenger.


"Lakini bado hawajiamini vya kutosha kwa sababu ya tukio lililowakuta Afrika Kusini. 

Mategemeo kwa Ufaransa ni madogo kwa sababu ya jambo hilo, lakini wana uwezo.

"Wana wachezaji nyota kama Benzema, (Franck) Ribery, (Samir) Nasri. Kama wakiandaliwa vizuri kisaikolojia naweza kuwashangaza wengi kwenye michuano hiyo."