![]() |
West mwenye jezi ya kijana akionyesha cheche zake |
Mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya England na klabu ya Everton, Gordon West afariki dunia akiwa na miaka 69 baada ya kusumbuliwa na maladhi kwa muda mrefu.
West alikaa Goodison Park kwa miaka 11 huku akicheza michezo zaidi ya 400 na alifanikiwa kushinda mataji 2 ya ligi mwaka 1963 na 1970, pia kombe la FA mwaka 1966.
Everton ilimsajili Gordon West kwa kitita cha pound za Uingereza 27,000 kutoka Blackpool na kuweka rekodi ya goli kipa kusajiliwa kwa pesa nyingi kwenye ligi ya England.
Pia kipa huyo alipata kushinda vikombe vitatu akiwa na England, na alikuwa moja kati ya wachezaji wa kikosi cha England kilichoshika nafasi ya tatu kwenye michuano ya Ulaya mwaka 1968. Hata hivyo baada ya miaka miwili West alikataa kwenda Mexico kushiriki kombe la Dunia na timu ya taifa ya England kwa kisingizio cha kutaka muda wa kutosha kukaa na familia yake.
Gordon West pia alipata kucheza timu jirani na Everton, Tranmere Rovers
No comments:
Post a Comment