Kocha aliyechukua mikoba kwa muda baada ya kufukuzwa kwa Andres Villa Boas Chelsea, Di Matteo amesaini mkataba wa miaka miwili kukinoa kikosi hicho tokea jijini London.
Di Matteo, 42 alichukua jukumu la kuinoa Chelsea kwa mkataba wa muda mfupi baada ya aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo kufukuzwa kazi. Di Matteo alishinda vikombe viwili akiwa kama kocha wa muda wa Chelsea, Kombe la FA Cup na lile la Klabu Bingwa barani Ulaya.
Mchezaji huyo wa Italy pia Chelsea mapema jumatano hii baada ya kutangazwa kuwa kocha wa kudumu amesema "Nina furaha sana kuchaguliwa kama kocha mkuu wa kikosi cha kwanza"
"Wote kwa pamoja tulipata mafanikio makubwa msimu uliopita kitu kilichoweka historia kwa klabu hii kubwa duniani. Lengo letu ni kuendeleza kile tulichokipata na nimejiandaa vizuri kwa ajiri ya maandalizi ya msimu ujao" aliongeza kusema Di Matteo
Uwezo wa Di Matteo umeweza kuonekana baada ya kuifanya Chelsea kuwa klabu ya kwanza toka jiji la London kuweza kushinda kombe la UEFA Champions League.
No comments:
Post a Comment