![]() |
Dinho kazini |
Baada ya kubwaga manyanga kwenye klabu yake ya Flamengo kutokana na madai ya mshahara wake mapema week iliyopita, kiungo wa kimataifa wa Brazili amesaini mkataba wa kuichezea timu ya Atletico Mineiro pia ya nchini Brazili.
Taarifa zilizothibitishwa na klabu hiyo ya Atletico Mineiro zimeeleza kuwa mchezaji huyo amesaini mkataba utakao mfanya acheze kwenye timu hiyo hadi mwishoni mwa mwaka huu.
Ronaldinho, 32 mara baada ya kusitisha mkataba wake na timu ya Flamengo alihusishwa na taarifa za kwenda kucheza soka lake nchini Uchina kwenye klabu ya Guangzhou Fuli pia alihusishwa na kuhamia timu ya Palmeiras.
Lakini taarifa za Gaucho kusaini mkataba na Atletico Mineiro zinaondoa uvumi huo uliomhusisha mchezaji huyo mara baada ya kubwaga manyanga timu ya Flamengo.
No comments:
Post a Comment