Pages

Thursday, 7 June 2012

KOCHA MPYA WA VILLARREAL AFARIKI DUNIA KABLA YA KUANZA KIBARUA CHAKE

Manolo Preciado
Manolo alikifundisha kikosi cha Sporting Gijon kwa miaka 6
 Kocha mpya aliyechaguliwa na timu ya Villarreal kwa ajiri ya kikinoa kikosi chake kuanzia mwanzoni mwa msimu ujao Manolo Preciado amefariki dunia asubuhi ya leo baada ya kusumbuliwa na tatizo la moyo [heart attack].

Kocha huyo wa zamani wa Sporting Gijon amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 54, gazeti la Marca la nchini Uhispania limelipoti.

Preciado, ndo kwanza alikuwa amekubali ofa ya kikinoa kikosi cha Villarreal kuanzia msimu ujao na alitegemea kutambulishwa rasmi kwa mashabiki na vyombo vya habari ijumaa ya kesho, siku moja kabla ya kifo chake.

Habari kwenye tovuti ya klabu ya Villarreal inasomeka "Kocha Manolo Preciado amefariki usiku wa manane mjini Valencia kutokana na shambulio la moyo"

"Villarreal inaeleza kwa masikitiko makubwa kuondokewa na mtu huyu na inatoa pole kwa familia yake na ndugu zake pia"


No comments:

Post a Comment