Pages

Sunday, 3 June 2012

RONALDINHO ABWAGA MANYANGA FLAMENGO

Gaucho katika moja ya mechi alizochezea Flamengo
Mchezaji wa zamani wa Fc Bacelona na kiungo mchezeshaji wa timu ya taifa ya Brazil Ronaldinho Gaucho amebwaga manyanga kwenye timu ya Flamengo aliyokuwa akiichezea baada ya mgogoro wa muda mrefu kuhusu malipo ya mshahara wake.

Ronaldinho amekuwa kwenye vita ya maneno na Flamengo kwa muda mrefu kuhusiana na madai yake hayo huku mchezaji huyo akieleza kutokuwa na amani klabuni hapo baada ya kufanyiwa vitendo visivyo vya kiungwana [ Rubro-Negro ] kwenye mchezo dhidi ya Internacional.

Mapema alhamisi hii Flamengo walipinga ripoti zilizoeleza kuwa kiungo huyo wa kimataifa wa Brazil yuko huru, hata hivyo hatua hiyo ilipelekea Ronaldinho, 32 kuchukua hatua zaidi za kisheria kwa kuishitaki timu yake akidai zaidi ya Euro milioni 16 za mshahara wake, bonasi na haki za picha [image rights]. Labour Court ya mjini Reo de Janeiro ilitoa iliyosikiliza kesi hiyo ilitoa maamuzi yenye manufaa dhidi ya Gaucho [gaucho alishinda kesi].

Nalo shirikisho la soka nchini Brazili (CBF) lilikuwa likisubiri uamuzi wa mahakama ili kumfanya Ronaldinho awe mchezaji huru.

Hata hivyo Vice-President wa Flamengo ameeleza kupata taarifa za hukumu ya mahakama hiyo ya Labour na kueleza nia ya klabu ya Flamengo kukata rufaa dhidi ya maamuzi ya mahakama.

No comments:

Post a Comment