Pages

Sunday, 27 May 2012

SPAIN NAYO YAWEKA HADHARANI SILAHA ZA MAANGAMIZI KUELEKEA EURO 2012

Vicenet del Bosque
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uhispania Vicente del Bosque (61) ametangaza kikosi chake cha wachezaji 23 kitakachoiwakilisha Uhispania kwenye michuano ya Uefa Euro 2012 nchini Poland na Ukraine.

Kocha huyo wa kihispania amewaacha Adrian Lopez toka Atletico Madrid na Roberto Soldado toka Valencia huku akifanya mabadiliko ya wachezaji 9 baada ya kuwajumuisha kundini wachezaji toka Barcelona na Athletic Bilbao waliocheza fainali ya Copa del Rey siku ya Ijumaa.

Kuachwa kwa Adrian Lopez aliyeonyesha mchezo wa kuvutia kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Serbia pamoja na kuachwa kwa Soldado kumewashangaza wadau wengi wa soka nchini Spain na dunia kwa ujumla. 

Mapema mwezi huu Vicente del Bosque alinukuliwa akisema kuwa Pedro atabaki nyumbani akitazama michuano hiyo kwenye luninga, hali imekuwa tofauti baada ya kocha huyo kumjumuisha mshambuliaji huyo toka Fc Barcelona hasa baada ya kufunga magoli mawili kwenye fainali ya Copa del Rey dhidi ya Bilbao.

Uhispania watatupa karata yao ya kwanza kwenye michuano hiyo ya Euro 2012 dhidi ya Italia (june 10) kabla ya kucheza na Jamhuri ya Ireland (june 14) na baadae Croatia (june 18)

Kabla ya kuanza kwa michuano hiyo, mabingwa hawa wa Dunia na Ulaya watacheza tena michezo yao ya kirafiki dhidi ya Korea Kusini na Uchina.

KIKOSI CHA UHISPANIA KUELEKEA UERO 2012

JinaKlabu
Makipa: 
Iker CasillasReal Madrid
Pepe ReinaLiverpool
Victor ValdesBarcelona
Mabeki: 
Raul AlbiolReal Madrid
Jordi AlbaValencia
Alvaro ArbeloaReal Madrid
Sergio RamosReal Madrid
Juanfran TorresAtletico Madrid
Gerard PiqueBarcelona
Javi MartinezAthletic Bilbao
Viungo/Midfielders: 
Sergio BusquetsBarcelona
XaviBarcelona
Andres IniestaBarcelona
Xabi AlonsoReal Madrid
Santi CazorlaMalaga
Cesc FabregasBarcelona
David SilvaManchester City
Jesus NavasSevilla
Juan MataChelsea
Washambuliaji: 
PedroBarcelona
Alvaro NegredoSevilla
Fernando TorresChelsea
Fernando LlorenteAthletic Bilbao

No comments:

Post a Comment