Pages

Sunday, 27 May 2012

MIDO APIGWA CHINI ZAMALEK, HUKU SHEHATA AKISALIA KAMA KOCHA MKUU

Shehata akiwa kazini
Bodi ya timu ya Zamalek toka nchini Misri imeweka kando tofauti kati yake na kocha mkuu wa timu hiyo Hassan Shehata, kwa kumrudisha kundini kocha huyo aliyeomba kujiuzulu klabuni hapo.


Mwenyekiti wa klabu hiyo Mamdouh Abbas alitangaza jana jumamosi kuwa Shehata bado ni kocha mkuu wa timu hiyo na hawawezi kumwachia aondoke.


"tumekataa ombi lake la kujiuzulu, ni kocha wetu na bado ataendelea kuwa na sisi, kilichotokea wiki iliyopita ilikuwa ni kutokuelewana kwa mambo fulani lakini kwa sasa hali ni shwari" Abbas aliiambia supersport.com 


Habari zilizoenea kwenye vyombo vya habari nchini Misri wiki iliyopita zinaonyesha kuwa Shehata aliamua kujiuzulu baada ya bodi ya Zamalek kutokufanyia kazi maombi yake ya kuwachukulia hatua za kinidhamu wachezaji Ahmed Mido Hossam na Mahmoud Abd Al Razek "Shikabala"


Hata hivyo Bodi ya klabu hiyo imeamua kumtimua kwenye kikosi chake Mido na kumshukuru kwa mchango wake aliotoa kwa kipindi chote akiwa na Zamalek.


"hatumuhitaji Mido kwa sasa lakini tutamuhitaji badae siku atakapo stafu soka yake ili awe aje kuwa moja kati ya memba wa bodi ya Zamalek, tunaweza tukawa tumempoteza kama mchezaji lakini tunaamini hatutampoteza katika hali ya kibinadamu" Ibrahem Yousef ambaye ni memba wa bodi aliiambia pia supersport.com


Katika mwendelezo wa habari hii, bodi ya klabu hii pia imemtoa kwa mkopo Shikabala baada ya kutokea mtafaruku kati yake na kocha Shehata kwenye mchezo dhidi ya Maghreb Fes kwenye michuano ya klabu bingwa barani Afrika.


Zamalek itarudi tena kambini kuanzia tarehe mosi june mwaka huu.

No comments:

Post a Comment